Business

Wavuvi Kwale wadai kuhangaishwa na wavuvi wa Tanzania

Published

on

Wavuvi kaunti ya Kwale walalamikia kukandamizwa na wavuvi kutoka taifa jirani la Tanzania kufuatia  mizozo ya mipaka.

Kulingana nao wavuvi hao, wamekua wakinyanyaswa  na hata kutozwa  faini ya hadi shilingi milioni 4 wanapopatikana wakivua katika sehemu zinazodaiwa kuwa katika nchi ya Tanzania  na maafisa hao.

Juma Rama Yusuf mwenyekiti wa wavuvi eneo la Jimbo na mwenzake wa Vanga Ngoto Mohamed walisema kuwa wavuvi wa Tanzania wamepewa  uhuru wa kutekeleza shughuli za uvuvi humu nchini ili hali wenyeji wanahangaika.

Aidha waliitaka  serikali ya  Kenya  na ile ya Tanzania  kuja pamoja na kutatua swala la  mipaka katika bahari hindi ili kukomesha mizozo ya mara kwa mara inaoshuhudiwa kati ya wavuvi wa Kenya na maafisa walinda bahari kutoka Tanzania.

 Taarifa ya Pauline Mwango

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version