Business

Vijana Kaloleni Wahimizwa Kujiunga na SACCOs ili Kujitegemea Kimaisha

Published

on

Vijana eneo bunge la Kaloleni na Kilifi kwa ujumla wamehimizwa kujiunga kwenye mashirika ya akiba na mikopo ili kupata mtaji wa kuanzisha biashara ndogondogo zitakazowasaidia kujikimu kimaisha .

Kiongozi wa vijana katika wadi ya Kayafungo huko Kaloleni Kirau Brian Santa amesema vijana wana uwezo wa kujiendeleza kimaisha bila hata kuajiriwa endapo watajiunga katika vyama vya ushirika.
Aidha amewataka kujihusisha na kazi za mikono zikiwemo za ujenzi , jua kali miongoni mwa nyengine ili kujiendeleza na kujiinua kichumi.

Akizungumza na mwanahabari wetu,Brian amesema vijana wengi wametumiwa vibaya na baadhi ya viongozi kutokana na kutojituma.

“vijana tujiunge na mashirika ya akiba na mikopo ili tupate mtaji utakatuwezesha kufanya biashara ndogo ndogo ili kujiendeleze kimaisha na kuepuka kutumiwa vibaya na baadhi ya viongozi.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version