News

Utoaji Huduma wa SHA Unachangamoto, Asema Waziri wa Afra

Published

on

Waziri wa Afya nchini, Deborah Barasa, amekiri kuwepo na changamoto za utoaji wa huduma za afya kupitia mfumo mpya wa bima ya afya nchini SHA.

Waziri Deborah amesema tayari wadau wa sekta ya Afya nchini kwa ushirikiana na serikali wako mbioni kuhakikisha wanashughulikia changamoto hizo ili kuwawezesha wananchi kupata huduma bora za afya kupitia SHA.

Akizungumza na Wanahabari, Waziri Deborah ameweka wazi kwamba licha ya changamoto hizo kushuhudiwa katika maeneo mbalimbali nchini mikakati bora imeidhinishwa ili kuhakikisha huduma zote za afya zinaimarishwa vyema.

Haya yamejiri baada ya hospitali za kibinafsi za zile za kidini nchini zikidai kwamba zitasitisha utoaji wa huduma za afya kupitia bima ya Afya ya SHA kuanzia siku ya Jumatatu wakisema wanadai SHA zaidi ya shilingi bilioni 30.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version