News

Ukosefu wa vitambulisho changaoto kwa usajili wa walemavu

Published

on

Ukosefu wa vitambulisho vya kitaifa pamoja na vyeti vya kuzaliwa ni changamoto inayoathiri shughuli ya usajili wa watu wanaoishi na uwezo maalum kaunti ya Kwale.

Haya yametajwa na Mshirikishi wa Shirika la Muslim Women Advancement of Rights & Protection (MWARP) Mwalimu Ali, ambaye alisema wanalenga kutatua changamoto hiyo kwa kuihusisha Ofisi ya usajili wa stakabadhi hizo muhimu.

Akizungumza wakati wa zoezi la usajili wa jamii ya walemavu katika eneo la Kilimangodo eneo bunge la Lungalunga kaunti ya Kwale, Ali alisisitiza umuhimu wa stakabadhi hizo kwa jamii za mashinani.

“Tunaendelea na hamasa mashinani kwa ushirikiano na ofisi ya usajili wa vitambulisho vya kitaifa na vyeti vya kuzaliwa ili kuhakikisha jamii ya walemavu wanapata stakabadhi hiyo na kusajiliwa rasmi ili kunufaika na huduma muhimu za serikali”, alisema Ali.

Kwa upande wao jamii ya walemavu eneo hilo wamelipongeza Shirika hilo kwa kuanzisha mpango na kusema kwamba kuna haja ya wahisani mbalimbali kujitokeza na kuwasaidia ili wajiendeleze.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version