Sports

Uganda Cranes Yaangukia Pabaya Katika Mchezo wa Ufunguzi wa CHAN

Published

on

Timu ya taifa ya Uganda Cranes yaanza vibaya kipute cha CHAN baada ya kutiwa darasani, kabila ya kuchabangwa magoli 3-0 na The Desert foxes mechi ya ufunguzi ugani Nelson Mandela Stadium mjini Kampala hapo jana.

Wageni walichukua uongozi wa mapema kupitia mshambulizi Ayoub Ghezela dakika ya 36 kabila kuongeza goli la pili dakika ya 76 kipindi cha pili kupitia mshambulizi wa CR Belouzidad Abderahmene Meziane kabila ya Sofiane Bayazid kufunga la tatu dakika tatu badaye,na kuzamisha meli la Cranes ambao walikua wameahidiwa donge nono pesa milioni 43 kwa kila ushindi na Rais Yoweri Museveni.

Katika mechi nyingine;Guinea walianza vema kwa kunyuka Niger goli 1-0 katika uwanja huo uo.

Katika ratiba ya leo ni kwamba mabingwa watetezi Senegal ‘The Lions Of Teranga’watamenyana na ‘The Super Eagles’ Ya Nigeria saa mbili usiku ugani Amaan Complex Zanzibar.

Mechi ya kwanza itahusisha Congo dhidi ya Sudan saa kumi na mbili jioni.

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version