Business
Tezo: Wakulima Watarajia Mavuno Tele ya Mahindi
Wakulima wa mahindi humu nchini wanasema kuwa wanatarajia mavuno bora mwaka huu ikilinganishwa na mwaka jana.
Kulingana na wakulima hao mvua inayoendelea kunyesha kote nchini inawapa matumaini kupata mavuno mengi mno ikilinganishwa na msimu uliopita.
Wakizungumza na cocofm wakulima hao kutoka eneo la Tezo kaunti ya kilifi wamesema kuwa bei ya mahindi inatarajiwa kuteremka kwani mahindi yatakuwa yanapatikana kwa wingi hali ambayo itawapa wananchi afueni.
Hata hivyo wameitaka serikali kuweka mikakati ya kununua mahindi kutoka kwao na kwa bei nzuri ili kuwainua kiuchumi.