News

Serikali ya kaunti ya Kilifi yaagizwa kusitisha utekelezaji wa bima ya matibabu

Published

on

Mahakama ya Malindi kaunti ya Kilifi imetoa amri ya kusitishwa kwa utekelezwaji wa bima ya matibabu ambayo inapeanwa na serikali ya kaunti ya Kilifi.

Hii ni baada ya watu wawili kufikisha kesi mbele ya mahakama hiyo wakilalamikia namna harakati za kumtafuta mkandarasi wa bima hiyo zilivyofanywa.

Walalamishi hao Dishan Joel Mwanyumba na Edward Aranga wanasema shughuli hiyo haikufanywa kwa uwazi na aliyekabidhiwa kandarasi hiyo alikuwa amechaguliwa kabla ya kutangazwa kwa kandarasi hiyo.

picha kwa hisani/Mahakama ya Malindi

Kupitia wakili wao Omayo Aranga walalamishi hao wanasema kandarasi hiyo ya zaidi ya shilingi milioni 500 imekuwa na vigezo vigumu ambavyo vinafungia nje kampuni nyingi hasa kigezo cha malipo ya zaidi ya shilingi bilioni 2 katika mwaka wa fedha wa 2023 kwa kampuni ambazo zilituma maombi ili kupata kandarasi hiyo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version