Sports

Sare Tasa na Burkina Faso Yaahirisha Ndoto za Misri Kufuzu Kombe la Dunia

Published

on

Matumaini ya taifa la Misri la kufuzu Kombe la Duniabado  baada ya kutoka sare tasa ya 0-0 dhidi ya Burkina Faso kwenye mechi ya Kundi A iliyochezwa Ouagadougou, Jumanne.

Kikosi cha Hossam Hassan ambacho hakijapoteza mchezo wowote kimefikisha pointi 20 na kuongoza Kundi A kwa tofauti ya pointi tano dhidi ya Burkina Faso, huku kukiwa na mechi mbili pekee zikisalia kwenye mchujo.

Kwa kuwa ni washindi wa makundi pekee wanaofuzu moja kwa moja, mabingwa wa Afrika mara saba wanahitaji alama mbili pekee kutoka kwa michezo yao miwili ya mwisho ili kujihakikishia nafasi na kufanikisha ushiriki wao wa nne kwenye Kombe la Dunia. Watakutana na Djibouti na Guinea-Bissau mwezi Oktoba.

Kocha wa Misri, Hassan, hata hivyo, alisherehekea matokeo hayo ambayo yamewasogeza hatua moja karibu na kufuzu katika mashindano makubwa ya timu 48 yatakayofanyika Amerika Kaskazini mwaka ujao.

“Ni siku kubwa kwa watu wa Misri… Ningependa kuwashukuru kila mchezaji kwa juhudi zao dhidi ya timu ngumu ambayo ina wachezaji wanaocheza Premier League, Bundesliga na Ligue 1,” alisema Hassan, mshambuliaji wa zamani wa Misri aliyewaongoza kufuzu Kombe la Dunia mwaka 1990, akizungumza na kituo cha On Sport.

“Licha ya kucheza ugenini Burkina Faso, tulicheza kwa mtindo chanya na kuunda nafasi kubwa. Wakati huohuo, tulidumisha uwiano. Tungelikuwa tumefunga goli moja au mawili kabla ya mwisho,” aliongeza.

Misri ilipata pigo mapema baada ya mshambuliaji wa Manchester City, Omar Marmoush, kulazimika kutoka nje kwa majeraha dakika ya 9.

Fursa yao bora ilikuja dakika ya 67 wakati Mohamed Salah alipompasia Osama Faisal lakini shuti lake likakataliwa kwa kuotea. Trezeguet wa Misri alikosa nafasi ya kwanza ya mchezo baada ya jaribio lake kuokolewa na kipa wa Burkina Faso, Herve Koffi.

Wenyeji hawakuwa na mashambulizi mengi, huku mshambuliaji wa Sunderland, Bertrand Traore, akiongoza juhudi zao bora.

Misri walikaribia kufunga goli la ushindi dakika za mwisho, lakini Mostafa Mohamed alipoteza nafasi mbili muhimu.

Hassan, ambaye ndiye mfungaji bora wa muda wote wa Misri, anatarajiwa kuwa wa kwanza kuongoza taifa hilo kufika Kombe la Dunia akiwa mchezaji na pia kocha.

Kocha huyo mwenye umri wa miaka 59 alisema: “Lengo langu lilikuwa kufundisha timu ya taifa ya Misri. Nimekuwa nikiota kila mara jambo hilo. Nataka kutimiza ndoto ya mashabiki na kuishi kwa imani yao (kwa kuongoza timu kufuzu Kombe la Dunia).”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version