News

Macharia: Jamii ya Kilifi kusini watapeliwa ardhi kufuatia ukosefu wa Elimu

Published

on

Msaidizi wa Kamishna wa kaunti ya Kilifi eneo la Kilifi Kusini, Francis Macharia amesema ukosefu wa elimu umechangia kwa wanajamii wengi kaunti ya Kilifi kutapeliwa katika umiliki wa ardhi.

Akizungumza eneo la Vipingo, Macharia alisema kuwa wanajamii wengi hasa wazee wamekuwa wakitapeliwa mashamba yao kutokana na kukosa kisomo.

Macharia alisisitiza haja ya jamii kuzingatia elimu kwani visa vya ulaghai wa mashamba kutokana na ukosefu wa elimu vimekithiri mno hasa mashanani.

“Kuna baadhi ya vijana pia wamekuwa wakiwatapeli wazazi wao fedha za inua jamii pindi zinapotumwa, na hii imechangiwa na kutosoma wazee hao” aliongeza Macharia.

Macharia alisema wazazi pia wanapaswa kuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa wanao wanapata elimu ipasavyo akisema kuwa eneo la Kilifi kusini limekuwa na visa vingi vya watoto wanaoacha shule na kuingilia vibarua.

Taarifa ya Hamis Kombe

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version