Sports

Rais Atoa Ahadi Nono Kwa Stars Kuelekea Mechi Ya Jumapili

Published

on

Rais William Ruto ametangaza kuwa kila mchezaji wa timu ya taifa atapokea shilingi milioni 2.5 kama marupurupu endapo wataibuka na ushindi kwenye mechi ya mwisho dhidi ya Zambia, Jumapili hii. Hii ni ongezeko la shilingi milioni 1.5 kutoka kiwango cha awali.

Rais alitoa ahadi hiyo alipowatembelea wachezaji katika hoteli yao jijini Nairobi, na kuongeza kuwa kila mchezaji atapewa shilingi milioni 1 watakapofika robo fainali, pamoja na nyumba ya vyumba viwili katika mradi wa nyumba za bei nafuu, popote watakapochagua.

Ahadi hizi zinakuja kufuatia ushindi muhimu wa goli 1–0 uliopatikana jana dhidi ya Morocco katika mechi ya tatu ya michuano ya Kombe la CHAN iliyochezwa Uwanja wa Kasarani.

Bao pekee la mchezo huo lilifungwa na mshambulizi wa klabu ya Tusker FC, Ryan Wesley Ogam, katika dakika ya 41 ya kipindi cha kwanza, na kuifanya timu ya taifa kuongoza Kundi A kwa alama 7 baada ya mechi tatu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version