News
Prof Kindiki: Uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2027 utakuwa huru, haki na amani
Naibu Rais Prof Kithure Kindiki amewahakikishia wakenya kwamba uchaguzi mkuu ujao wa mwaka wa 2027 utakuwa huru, haki na amani.
Kindiki amemshtumu Kinara wa Chama cha Democracy for the Citizen’s Party {DCP} Rigathi Gachagua, akisema kauli alizozitoa kuhusu uchaguzi mkuu ujao zinalenga kuligawanya taifa kwa msingi ya vurugu.
Kindiki amewataka wakenya kuwa makini na viongozi wasio na ajenda ya maendeleo kwa wananchi na badala yake kushirikiana na serikali ili kuhakikisha miradi ya maendeleo inatekelezwa mashinani.
Wakati huo huo amewahakikishia wakenya kwamba serikali ya Kenya kwanza iko mbioni kuhakikisha inakabiliana na changamoto za gharama ya maisha, akiwataka wapinzani kuipa nafasi serikali kuwajibikia majukumu yake.
Baba Yaga
May 19, 2025 at 9:44 pm
Hii Imeenda