News
Papa Leo XIV amteua Askofu wa kwanza kutoka China
Makao makuu ya Kanisa Katoliki duniani mjini Vatican ilitangaza uteuzi wa kwanza wa Askofu mwenye asili ya China chini ya usimamizi wa Papa Leo XIV.
Hii inaashiria uungaji mkono wa Papa mpya kwa makubaliano yenye utata juu ya uteuzi uliyopingwa na mtangulizi wake na Beijing.
Ofisi ya Vatican imeeleza kuridhishwa na China kwa kutambua kuteuliwa kwa Joseph Lin Yuntuan kama Askofu msaidizi wa Fuzhou, mji mkuu wa jimbo la Fujian kusini mashariki.
Papa alifanya uteuzi huo tarehe 5 mwezi Juni mwaka huu wa 2025.
“Tukio hili linawakilisha matunda zaidi ya mazungumzo kati ya kiti kitakatifu na Mamlaka ya China na ni hatua muhimu katika safari ya Jumuiya ya dayosisi,” ilisema katika taarifa.
Uongozi wa Vatican na ule wa Kikomunisti wa China hauna uhusiano rasmi wa kidiplomasia, kwani Vatican inaitambua Taiwan huku Beijing ikidai kisiwa hicho kinachojitawala ni eneo lake.
Lakini katika makubaliano ya kihistoria, walikubaliana mwaka 2018 kuruhusu pande zote mbili kuwa na usemi katika kuwataja maaskofu nchini China, ambayo ina takriban Wakatoliki milioni 12.
Hata hivyo hayati Papa Francis alipokuwa akitafuta nafasi ya Kanisa kuingia nchini China, mkataba huo ulifanywa upya mara kadhaa, wa hivi karibuni ikiwa ni mnamo Oktoba 2024, baada ya mda wa miaka minne.
Papa Francis alifariki Aprili 21 mwaka 2025 baada ya miaka 12 ya kuhudumu kama Kiongozi wa waumini wa Kanisa katoliki duniani wapatao bilioni 1.4 na Papa Leo alichaguliwa katika kongamano la Makadinali Mei 8 mwaka 2025.
Taarifa ya Joseph Jira