News

Oscar Wanje Awakashifu Wawakilishi Wadi Wenza

Published

on

Mwakilishi wadi wa Ganda, kaunti ndogo ya Malindi, kaunti ya Kilifi, Oscar Wanje amekemea vikali tukio ambapo wawakilishi wadi wawili walihusika katika mshikemshike wa kumpiga mwakilishi wadi maalum, Elina Mapenzi, baada ya kutofautiana bungeni.

Akizungumza kupitia mtandao wake wa kijamii, Wanje amesema kuwa kitendo hicho kilidhihirisha utovu wa nidhamu lakini pia dhulma dhidi ya wanawake ikizingatiwa kwamba wawakilishi wadi hao waliompiga Mapenzi walikuwa wa kiume.

Wanje amekitaja kitendo hicho kama ukiukaji wa demokrasia kwani kuna uhuru wa viongozi kutofautiana katika maswala mbalimbali.

Ni mvutano ambao ulimpelekea Mapenzi kupata majeraha.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version