News

NGEC, yasisitiza udhibiti wa dhulma za kijinsia

Published

on

Tume ya jinsia na usawa NGEC inasisitiza umuhimu wa kuwashirikisha wanaume ili kudhibiti visa vya dhuluma za kijinsia nchini.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa mkakati wa miaka mitano ya tume hiyo, Waziri wa jinsia nchini Hanna Cheptumo alisikitishwa na ongezeko la visa vya ukatili wa kijinsia na kusisitiza umuhimu wa kuwahusisha vijana na watu walio na uatilifu ili kudhibiti dhuluma mbalimbali na kuleta usawa katika jamii.

Vile vile, Cheptumo alishinikiza uwekezaji kwenye miradi ya kuwawezesha kiuchumi wanawake, watu walio na uatilifu na vijana.

Cheptumo alisema iwapo watu walio na uatilifu, vijana na wanawake watawezeshwa ipasavyo wataweza kujikimu kimaisha na hata familia zao bila kutegemea misaada na kusisitiza kwamba hakuna mtu yeyote ambaye anapaswa kubaguliwa kwa namna yoyote ile.

“Kifungu cha 27 cha Katiba ya nchi ya mwaka wa 2010, inampa kila mtu haki ya usawa na uhuru dhidi ya ubaguzi wa aina yoyote’’ Alisema Cheptumo.

Kwa upande wake msemaji wa serikali Isaac Mwaura alitoa wito kwa watu walio na uatilifu kuweka juhudi zaidi katika kujiendeleza kimaisha badala ya kusubiri msaada kutoka kwa mashirika mbalimbali na serikali huku akiwataka kujikubali na kupuuza yale ambayo yanasemwa kuhusu hali zao kwani wana uwezo kama wanadamu wengi.

“Kama watu walio na uatilifu mtapitia unyanyapaa mwingi kutoka kwa watu hasa mnapopata nafasi za uongozi kwa sababu kuna watu wanaona hamstahili’’ alisema Mwaura.

Taarifa ya Janet Mumbi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version