Connect with us

News

NGEC, yasisitiza udhibiti wa dhulma za kijinsia

Published

on

Tume ya jinsia na usawa NGEC inasisitiza umuhimu wa kuwashirikisha wanaume ili kudhibiti visa vya dhuluma za kijinsia nchini.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa mkakati wa miaka mitano ya tume hiyo, Waziri wa jinsia nchini Hanna Cheptumo alisikitishwa na ongezeko la visa vya ukatili wa kijinsia na kusisitiza umuhimu wa kuwahusisha vijana na watu walio na uatilifu ili kudhibiti dhuluma mbalimbali na kuleta usawa katika jamii.

Vile vile, Cheptumo alishinikiza uwekezaji kwenye miradi ya kuwawezesha kiuchumi wanawake, watu walio na uatilifu na vijana.

Cheptumo alisema iwapo watu walio na uatilifu, vijana na wanawake watawezeshwa ipasavyo wataweza kujikimu kimaisha na hata familia zao bila kutegemea misaada na kusisitiza kwamba hakuna mtu yeyote ambaye anapaswa kubaguliwa kwa namna yoyote ile.

“Kifungu cha 27 cha Katiba ya nchi ya mwaka wa 2010, inampa kila mtu haki ya usawa na uhuru dhidi ya ubaguzi wa aina yoyote’’ Alisema Cheptumo.

Kwa upande wake msemaji wa serikali Isaac Mwaura alitoa wito kwa watu walio na uatilifu kuweka juhudi zaidi katika kujiendeleza kimaisha badala ya kusubiri msaada kutoka kwa mashirika mbalimbali na serikali huku akiwataka kujikubali na kupuuza yale ambayo yanasemwa kuhusu hali zao kwani wana uwezo kama wanadamu wengi.

“Kama watu walio na uatilifu mtapitia unyanyapaa mwingi kutoka kwa watu hasa mnapopata nafasi za uongozi kwa sababu kuna watu wanaona hamstahili’’ alisema Mwaura.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Anselim, ashutumu utovu wa usalama Taita Taveta

Published

on

By

Kaimu Spika katika bunge la kaunti ya Taita Taveta Anselim Mwadime alieleza kusikitishwa na mauaji ya mhudumu mmoja wa bodaboda aliyeuliwa na kisha pikipiki yake kuchukuliwa katika eneo la chuo kikuu cha Taita Taveta.

Mwadime alisema kuna baadhi ya abiria ambao ni wahuni hubebwa na kisha kuwashambulia wahudumu wa pikipiki hadi kuwaua au hata kutoweka na pikipiki.

Aidha, Mwadime alisema kama viongozi wa kaunti ya Taita Taveta hawataruhusu visa hivyo kuendelezwa katika kaunti hiyo.

Vilevile, Mwadime aliishinikiza idara ya usalama kwenye kaunti ya Taita Taveta kuwajibika ipasavyo ili kudhibiti visa vya utovu wa usalama katika sekta ya bodaboda na wanaohusika wakabiliwe kisheria.

“Hili jambo linafaa kufuatiliwa kwa undani. Na tunalilaani vikali sisi kama viongozi wa Taita Taveta’’ alisema Mwadime.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Viongozi wahimizwa kushirikiana kubuni ajira kwa vijana

Published

on

By

Mwakilishi wa wadi ya Sabaki eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi Rose Baraka alitoa wito kwa viongozi wa kaunti ya Kilifi kushirikiana na mashirika ya kijamii pamoja na wawekezaji katika kaunti ya Kilifi ili kudhibiti changamoto za ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana.

Rose alisema hatua hiyo itasaidia pakubwa kuwaepusha vijana kujiingiza kwenye utumizi wa mihadarati sawa na uhalifu.

Akizungumza wakati wa kikao kilichowaleta pamoja maafisa wa shirika la SHOFCO pamoja na wakaazi wa Sabaki, Rose aliahidi kushirikiana na mashirika mbalimbali ya kijamii katika juhudi za kuwasadia wananchi kujiendeleza kupitia mpango wa ajira.

“Vijana ni wengi, kazi ni kidogo. Sisi kama viongozi tunastahili kutia bidii kutafuta haya mashirika ili tuangalie vijana wetu wasaidika vipi’’ alisema Rose Baraka.

Kwa upande wake Afisa wa Shirika la SHOFCO eneo la Magarini Kelvin Mtawali Karisa aliupongeza ushirikiano wa mwakilishi wa wadi huyo na shirika hilo na kuwataka vijana kujiunga kwenye makundi mbalimbali ili waweze kupata mikopo ya kujiendeleza kimaisha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending