Tume ya huduma ya Mahakama nchini (JSC) imemteua Jaji Mohammed Abdullahi Warsame kuwa Jaji wa Mahakama ya Upeo.
Mwenyekiti wa Tume hiyo ambaye pia ni Jaji mkuu nchini Martha Koome alisema jina la Jaji Warsame litawasilishwa kwa rais William Ruto ili kuteuliwa rasmi kwa kuambatana na Katiba na sheria nchini kisha kuliwasilisha bungeni kuidhinishwa rasmi.
Jaji Koome alisema Tume hiyo imezingatia masuala mbalimbali wakati wa mahojiano ikiwemo suala la uadilifu, uwajibikaji, usawa, hadhi ya kuwa jaji miongoni mwa masuala mengine kabla ya Tume hiyo kuridhia umuazi huo.
Jaji Warsame alikuwa miongoni mwa wakenya 5 waliotuma maombi ya kukuwa Jaji wa Mahakama ya upeo baada ya kifo cha Jaji Mohammed Ibrahim, Disemba mwaka 2025.

Mahojiano ya kutafuta nafasi Jaji wa Mahakama ya upeo katika Mahakama ya Milimani jijini Nairobi
Waliohojiwa katika nafasi hiyo ni pamoja na Jaji wa Mahakama kuu Katwa Kigen, na Francis Tuiyott pamoja na Jaji wa Mahakama kuu Joseph Sergon pamoja na aliyekuwa Mwenyekiti wa Mamlaka huru ya usimamizi wa maafisa wa Polisi (IPOA) Anne Waceke Makori.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
