Umoja wa mataifa wapunguza bajeti yake kwa bola milioni 577

Umoja wa mataifa wapunguza bajeti yake kwa bola milioni 577

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amependekeza kupunguzwa kwa bajeti ya umoja huo ya mwaka ujao kwa dola milioni 577, hatua ambayo itapunguza asilimia 18 ya kazi.

Akizungumza mbele ya kamati ya bajeti ya Baraza kuu la umoja wa mataifa, Guterres alisema umoja huo bado haujapokea mchango wa karibu dola milioni 900 kutoka kwa wanachama mwaka huu wa 2025.

Umoja wa mataifa unapendekeza bajeti ya dola bilioni 3 kwa mwaka 2026, ikiwa na upungufu wa asilimia 15 ikilinganishwa na bajeti ya mwaka huu.

Umoja wa Mataifa unakabiliwa na mgogoro wa kifedha uliosababishwa pakubwa na hatua ya Marekani kutolipa ada yake, kutokana na sera mpya za Rais Donald Trump.

Hatua hii ya umoja wa mataifa huenda ukachangia changamoto kubwa kwa mataifa wanachama hasa yanayotegemea pakubwa juhudi za umoja huo katika masuala mbalimbali ikiwemo usalama.