News

Mwili na mafuvu mawili yapatikana karibu na Shakahola

Published

on

Maafisa wa polisi kaunti ya Kilifi wamewaokoa watu wanne katika kijiji cha kwa Binzaro kilomita 6 kutoka Shakahola.

Kamishna wa kaunti ya Kilifi Josephat Biwot alisema oparesheni hiyo iliyohusisha wakaazi, watu watatu kati ya wanne waliookolewa wameonekana wakiwa dhaifu kuliko hali yao ya kawaida.

Mwili mmoja na mafuvu mawili ya binadam pia yamepatikana nyumbani humo.

Biwot alidokeza kuwa wahusika hawakupatikana nyumbani wakati wa oparesheni hiyo na haijabainika kilichokuwa kikiendelea.

Mwili na mafuvu hayo yalipelekwa katika hifadhi ya maiti ya katika hospitali ya kaunti ndogo ya Malindi.

Taarifa ya Joseph Jira

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version