Connect with us

News

Mwili na mafuvu mawili yapatikana karibu na Shakahola

Published

on

Maafisa wa polisi kaunti ya Kilifi wamewaokoa watu wanne katika kijiji cha kwa Binzaro kilomita 6 kutoka Shakahola.

Kamishna wa kaunti ya Kilifi Josephat Biwot alisema oparesheni hiyo iliyohusisha wakaazi, watu watatu kati ya wanne waliookolewa wameonekana wakiwa dhaifu kuliko hali yao ya kawaida.

Mwili mmoja na mafuvu mawili ya binadam pia yamepatikana nyumbani humo.

Biwot alidokeza kuwa wahusika hawakupatikana nyumbani wakati wa oparesheni hiyo na haijabainika kilichokuwa kikiendelea.

Mwili na mafuvu hayo yalipelekwa katika hifadhi ya maiti ya katika hospitali ya kaunti ndogo ya Malindi.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Rais Ruto: Wazazi tuchunge watoto wetu

Published

on

By

Rais William Ruto amewashauri wazazi kote nchini kuhakikisha wanawalekuza vijana wao katika mazingira ya maadili na uwajibikaji na wala sio kuwasukuma katika maisha ya kuhangaika.

Rais Ruto aliwahimiza wazazi, viongozi wa kisiasa na kidini kuhakikisha vijana wanazingatia maadili mema, kuwapa mazingira bora na kuhakikisha wanajitenga na makundi potovu.

Akizungumza baada ya kuhudhuria Ibada ya Jumapili katika Kanisa ya AIC Bomani katika kaunti ya Maachakos, Kiongozi wa nchi, alihimiza ushirikiano wa viongozi wote nchini ikiwemo wa kidini ili kuhakikisha wanawalida vijana kwani na nguzo kuu ya taifa.

“Watoto wetu ni zawadi kutoka kwa Mungu kwa familia zetu na taifa. Ni lazima tuwaelekeze, uzazi jukumu ulilopewa na Mungu”, tuachie Kanisa au serikali pekee jamani na tusikubali kuruhusu mtoto wako alelewe na wapiti njia”, alisema Rais Ruto.

Wakati huo huo aliwarai viongozi wa kisiasa kutowachochea vijana na kuzua vurugu sawa na kuharibu mali ya umma, akisema ni jukumu la wazazi, viongozi wa kidini na kisiasa kuwaelekeza vijana katika mwongozo bora.

Kauli yake imejiri baada ya taifa kuhushudia baadhi ya vijana wakipoteza maisha yao baada ya kupigwa risasi na maafisa wa polisi wakati wa makabiliana kati ya polisi na waandamanaji katika maeneo mbalimbali ya taifa.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Boniface Mwangi akamatwa na maafisa wa DCI

Published

on

By

Mwanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu nchini Boniface Mwangi amekamatwa na maafisa wa idara ya upelelezi wa jinai nchini DCI. 

Kulingana na Mkewe Boniface, Hellen Njeri Mwangi, Mumewe amekamatwa nyumbani wako katika eneo la Lukenya kaunti ya Machokos na maafisa waliojitambulisha kwamba wanatoka katika Idara ya DCI.

Hellen alisema Boniface amepelekwa katika makao makuu ya idara ya DCI jijini Nairobi huku sababu za kukamatwa kwa Boniface zikihusisha na masuala ya ugaidi.

Kulingana na Wakili wa Boniface, James Kamau alisema maafisa wa DCI walivamia makaazi ya mteja wake wakiwa wamejihami kwa silaha na kumtia nguvuni.

Hatua hii imejiri baada ya Boniface na Mwanaharakati kutoka Uganda Agather Utuhaire mnamo siku ya Ijumaa Julai 18, 2025 kuwasilisha kesi katika Mahakama ya Afrika Mashariki na kulishtaki taifa la Tanzania kwa madai kwamba maafisa wa serikali ya Tanzania walikiuka haki zao za kibinadamu.

Kwenye mashtaka hayo, Wanaharakati hao walidai kutekwa nyara na watu wasiojulikana wakiwa jijini Dar er Salam pamoja na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia na kutupwa nje ya mpaka wa Tanzania, Uganda na Kenya, mtawalia.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending