News

Mwaura: Hakuna Mswada wa Fedha wa Mwaka 2025 uliyowasilishwa Bungeni

Published

on

Serikali imejitokeza na kupinga taarifa zinazoendelea katika mitandao ya kijamii kwamba inalenga kuwasilisha mswada wa fedha wa mwaka wa 2025 bungeni ambao unalenga kuongeza ushuru kwa wakenya.

Msemaji wa Serikali Isaac Mwaura amesema taarifa hizo ni propaganda zisizo na ukweli wowote na ambazo zinalenga kuwagonganisha wakenya kama ilivyoshuhudiwa mwezi Juni mwaka wa 2024 wakati wananchi walipozua vurugu kupinga mswada wa fedha.

Katika kikao na Wanahabari katika jumba la mikutano la KICC jijini Nairobi, Mwaura amesema japo serikali iko na mipango ya kutengeneza bajeti ya mwaka wa kifedha wa 2025/2026, ni lazima wananchi wahusishwe kikamilifu katika vikao vya kutoa maoni ya umma.

Msemaji huyo wa serikali amebainisha kwamba serikali itahakikisha inawashikiza wakenya wanaokwepa kulipa ushuru kuwajibika huku akisema wakenya zaidi ya milioni 8.5 wamenufaika na bima ya Afya ya Taifa Care.

Wakati huo huo ameelezea hatua zilizopigwa na serikali za kimaendeleo katika kipindi cha zaidi ya miaka miwili sasa, akisisitiza haja ya wakenya kuunga mkono serikali kufanikisha ajenda yake ya maendeleo kwa wananchi wote.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version