News

KUPPET na KNUT washinikiza nyongeza ya mshahara

Published

on

Chama cha Walimu wa shule za upili na vyuo vya kadri nchini KUPPET, kimeionya Tume ya uajiri walimu nchini TSC dhidi ya kuwasilisha pendekezo lipya linalokinzana na mkataba wa makubaliano wa malipo wa CBA wa mwaka wa 2025-2029.

Katibu mkuu wa KUPPET nchini, Akello Misori alisisitiza kwamba kuna haja ya kutathiminiwa upya kwa marupurupu yote ya walimu, akisema ni lazima mkataba huo unaangaliwe.

Akello alisema ili kuwawezesha walimu kutekeleza makujumu yao vyema, ni lazima serikali kupitia Tume ya kuajiri walimu nchini TSC kuangalia upya mkataba uliopo mezani na kuhakikisha matakwa ya walimu yanatekelezwa.

“Hivi karibuni kutatua na mazungumzo na muajiri wetu na sisi tuko na msimamo kwamba ni lazima nyongeza ya mshahara ya asilimia 50 na marupurupu ya walimu wanaofanyakazi katika mazingira magumu ya asilimia 30 pia iangaliwe upya”, alisema Akello.

Hata hivyo katika hafla tofauti, Naibu Mwenyekiti wa kitaifa wa chama cha walimu nchini KNUT Aggrey Namisi alisema iwapo hakutakuwa na mwafaka wowote kuhusu pendekezo hilo la CBA basi wataitisha mgomo wa kitaifa kuanzia mwezi Agosti.

“Sisi tuko tayari kufanya kazi lakini pia matakwa yetu ni lazima yaangaziwe na tunaiambia TSC kama itaendelea kugairi mambo yetu ya CBA mpya tutaambia walimu waanze mgomo mwezi Agosti na watakaoumia na wanafunzi wa gredi ya 9”, alisema Namisi.

Katibu mkuu wa KNUT Collins Oyoo

KUPPET na KNUT hata hivyo wanalenga kuweka mezani mahitaji mapya ya walimu wakati wa mazungumzo kati ya serikali na viongozi wakuu wa vyama hivyo huku suala la nyongeza ya mishahara na marupurupu ya asilimia 50 likipewa kipau mbele.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version