Connect with us

News

KUPPET na KNUT washinikiza nyongeza ya mshahara

Published

on

Chama cha Walimu wa shule za upili na vyuo vya kadri nchini KUPPET, kimeionya Tume ya uajiri walimu nchini TSC dhidi ya kuwasilisha pendekezo lipya linalokinzana na mkataba wa makubaliano wa malipo wa CBA wa mwaka wa 2025-2029.

Katibu mkuu wa KUPPET nchini, Akello Misori alisisitiza kwamba kuna haja ya kutathiminiwa upya kwa marupurupu yote ya walimu, akisema ni lazima mkataba huo unaangaliwe.

Akello alisema ili kuwawezesha walimu kutekeleza makujumu yao vyema, ni lazima serikali kupitia Tume ya kuajiri walimu nchini TSC kuangalia upya mkataba uliopo mezani na kuhakikisha matakwa ya walimu yanatekelezwa.

“Hivi karibuni kutatua na mazungumzo na muajiri wetu na sisi tuko na msimamo kwamba ni lazima nyongeza ya mshahara ya asilimia 50 na marupurupu ya walimu wanaofanyakazi katika mazingira magumu ya asilimia 30 pia iangaliwe upya”, alisema Akello.

Hata hivyo katika hafla tofauti, Naibu Mwenyekiti wa kitaifa wa chama cha walimu nchini KNUT Aggrey Namisi alisema iwapo hakutakuwa na mwafaka wowote kuhusu pendekezo hilo la CBA basi wataitisha mgomo wa kitaifa kuanzia mwezi Agosti.

“Sisi tuko tayari kufanya kazi lakini pia matakwa yetu ni lazima yaangaziwe na tunaiambia TSC kama itaendelea kugairi mambo yetu ya CBA mpya tutaambia walimu waanze mgomo mwezi Agosti na watakaoumia na wanafunzi wa gredi ya 9”, alisema Namisi.

Katibu mkuu wa KNUT Collins Oyoo

KUPPET na KNUT hata hivyo wanalenga kuweka mezani mahitaji mapya ya walimu wakati wa mazungumzo kati ya serikali na viongozi wakuu wa vyama hivyo huku suala la nyongeza ya mishahara na marupurupu ya asilimia 50 likipewa kipau mbele.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

IEBC inaendelea kutambua vituo vya kusajili wapiga kura

Published

on

By

Maafisa wa tume ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC wamesema wanaendelea na zoezi la kutambua sehemu za kuweka vituo vya kusajili wapiga kura hasa maeneo ya mashinani.

Afisa msimamizi wa tume ya IEBC eneo bunge la Ganze kaunti ya Kilifi, Mohammed Bahero Aboud alisema juhudi hizo ni kuhakikisha zoezi la usajili wapiga kura litakaloanza rasmi Septemba 29, mwaka huu linafaulu.

Akizungumza mjini Kilifi, Bahero alisema tume hiyo inatumia mbinu mpya ya kutambua vituo vya jadi vya usajili wapiga kura na kuweka vituo vipya kulingana na mapendekezo ya sheria.

Wakati huo huo alidokeza kwamba tume ya IEBC imekuwa ikihamashisha wakenya kutokubali kushawishiwa na wanasiasa na kujisajili katika maeneo yasiokuwa yao hasa msimu huu ambao zoezi hilo linakaribia kuanza.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Kaunti ya Mombasa kukumbatia matumizi ya mfumo wa miale ya jua

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Mombasa imesema imeanza kutekeleza mpango wa kutumia nishati mbadala katika vituo vyote vya huduma za kaunti, kwa kuanza na mabadiliko ya mfumo wa taa hadi kutumia umeme wa miale ya jua.

Kwa mujibu wa waziri wa kawi, rasilimali asili na ustahimilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi kaunti ya Mombasa, Emily Achieng, hatua hii inalenga kupunguza gharama za matumizi ya umeme na kuhimiza matumizi ya nishati safi na rafiki kwa mazingira.

Mbali na hilo, waziri huyo alisema kaunti inaendelea kuweka vifaa maalum vya kupima ubora wa hewa katika maeneo mbalimbali ya mji na ndani ya taasisi za umma.

Lengo ni kupata ushahidi wa kisayansi kuhusu kiwango cha uchafuzi wa hewa, na kuchukuliwa kwa hatua za kisheria kwa wanaokiuka sheria.

Vifaa hivyo tayari vimewekwa katika hospitali ya rufaa ya Coast General na baadhi ya shule ikiwa ni sehemu ya mpango wa muda mrefu wa kaunti, kujenga ustahimilivu dhidi ya madhara ya mabadiliko ya tabianchi.

Mikakati hiyo pia itasaidia kaunti katika kufanya maamuzi kuhusu maeneo yanayofaa kuwekwa biashara fulani, ili kulinda wananchi dhidi ya maradhi yanayosababishwa na uchafuzi wa hewa.

Taarifa ya Mwanahabari wetu.

Continue Reading

Trending