News

Chibule, ahimiza wakaazi kutoa damu kusaidia wagonjwa wa Selimundu

Published

on

Wizara ya afya kaunti ya Kilifi imefichua kwamba maradhi ya Selimundu ni miongoni mwa maradhi ambayo yanaathiri idadi kubwa zaidi ya wakaazi kaunti hiyo.

Akiongea kwa niaba ya Waziri wa Afya kaunti hiyo Peter Mwarogo, mkurugenzi wa afya kaunti ya Kilifi Leli Hassan alisema kwamba kila siku zaidi ya watu kumi hupatikana wakiugua maradhi hayo kaunti ya Kilifi.

Akizungumza wakati wa maadhimisho ya maradhi hayo ya Selimundu katika uwanja wa Vipingo eneo bunge la Kilifi Kusini kaunti ya Kilifi, wizara hiyo imesema kwamba asilimia sitini ya maradhi hayo yameathiri wakaazi wa eneo bunge la Kilifi Kusini.

Kauli hiyo iliungwa mkono na Naibu Gavana kaunti ya Kilifi Florah Mbetsa Chibule ambaye alisisitiza haja ya wakaazi kujitokeza na kutoa damu kwa hiari ili kuhakikisha wanasaidia waathiriwa wanaougua maradhi ya Selimundu.

Wananchi wakishiriki maandimisho ya siku ya Selimundu

Vile vila Chibule alisitiza haja ya wakaazi kujisahili kwenye mpango wa bima ya Kitaifa ya afya SHA ili kupata matibabu ya gharama ya chini wanapotaka dharura ya kiafya.

Naibu gavana huyo alisistiza jamii kaunti hiyo kuondoa unyanyapaa kwa waathiriwa wa maradhi hayo huku akishinikiza hamasa kwa jamii kuhusu kwa watu wanaoishi na maradhi hayo.

Kwa upande wake mkurugenzi wa idara ya afya ya jamii Bashir Isaak akizungumza kwa niaba ya waziri wa afya nchini Aden Duale, alisema eneo la pwani na magharibi mwa nchi ndiyo yaliyosajili idadi kubwa ya wanaoishi na maradhi hayo.

Bashiri alipendekeza wahudumu wa afya nyanjani kupewa mafunzo maalumu ya kuhakikisha wanatambua sawa na kuwa na uwezo wa kutoa huduma kwa waathiriwa wa maradhi hayo hasa maeneo ya mashinani.

Alisistiza haja ya waathiriwa wa maradhi hayo na umma kwa ujumla kujisajili kwenye mpango wa bima ya matibabu ya afya wa SHA ili kuwagharamia matibabu kwani baadhi ya wanaougia maradhi hayo hawana uwezo wa kimatibabu sawa na kununua dawa.

Taarifa ya Joseph Jira

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version