News
Chibule, ahimiza wakaazi kutoa damu kusaidia wagonjwa wa Selimundu

Wizara ya afya kaunti ya Kilifi imefichua kwamba maradhi ya Selimundu ni miongoni mwa maradhi ambayo yanaathiri idadi kubwa zaidi ya wakaazi kaunti hiyo.
Akiongea kwa niaba ya Waziri wa Afya kaunti hiyo Peter Mwarogo, mkurugenzi wa afya kaunti ya Kilifi Leli Hassan alisema kwamba kila siku zaidi ya watu kumi hupatikana wakiugua maradhi hayo kaunti ya Kilifi.
Akizungumza wakati wa maadhimisho ya maradhi hayo ya Selimundu katika uwanja wa Vipingo eneo bunge la Kilifi Kusini kaunti ya Kilifi, wizara hiyo imesema kwamba asilimia sitini ya maradhi hayo yameathiri wakaazi wa eneo bunge la Kilifi Kusini.
Kauli hiyo iliungwa mkono na Naibu Gavana kaunti ya Kilifi Florah Mbetsa Chibule ambaye alisisitiza haja ya wakaazi kujitokeza na kutoa damu kwa hiari ili kuhakikisha wanasaidia waathiriwa wanaougua maradhi ya Selimundu.

Wananchi wakishiriki maandimisho ya siku ya Selimundu
Vile vila Chibule alisitiza haja ya wakaazi kujisahili kwenye mpango wa bima ya Kitaifa ya afya SHA ili kupata matibabu ya gharama ya chini wanapotaka dharura ya kiafya.
Naibu gavana huyo alisistiza jamii kaunti hiyo kuondoa unyanyapaa kwa waathiriwa wa maradhi hayo huku akishinikiza hamasa kwa jamii kuhusu kwa watu wanaoishi na maradhi hayo.
Kwa upande wake mkurugenzi wa idara ya afya ya jamii Bashir Isaak akizungumza kwa niaba ya waziri wa afya nchini Aden Duale, alisema eneo la pwani na magharibi mwa nchi ndiyo yaliyosajili idadi kubwa ya wanaoishi na maradhi hayo.
Bashiri alipendekeza wahudumu wa afya nyanjani kupewa mafunzo maalumu ya kuhakikisha wanatambua sawa na kuwa na uwezo wa kutoa huduma kwa waathiriwa wa maradhi hayo hasa maeneo ya mashinani.
Alisistiza haja ya waathiriwa wa maradhi hayo na umma kwa ujumla kujisajili kwenye mpango wa bima ya matibabu ya afya wa SHA ili kuwagharamia matibabu kwani baadhi ya wanaougia maradhi hayo hawana uwezo wa kimatibabu sawa na kununua dawa.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Waziri Joho na Mvurya waonya wanyakuzi wa ardhi.

Waziri wa madini na uchumi wa bahari nchini Ali Hassan Joho alisema serikali haitaruhusu tena wakaazi kufurushwa katika ardhi wanayoishi.
Akizungumza katika maeneo ya Mzambarauni mjini Mtwapa eneo bunge la Kilifi Kusini kaunti ya Kilifi, Joho alionya kwamba mabwenyenye wenye hulka ya kufurusha wananchi kwenye ardhi za umma kamwe hawataruhusiwa.
Joho alisema wananchi hawafai kuhangaishwa kwenye ardhi zao huku akiwatahadharisha maafisa wa serikali dhidi ya kushirikiana na mabwenyenye kuhangaisha raia kwenye ardhi zao.
Hii ni baada ya kuibuka malalamishi ya mabwenyenye kutaka kuwafurusha wakaazi wa Utange Kaunti ya Mombasa.
Kwa upande wake Waziri wa michezo na Sanaa nchini Salim Mvurya alidokeza kuwa serikali inapanga kununua mashamba ambayo hayatumiki ili kuyakabidhi ya wananchi.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Marekani yarusha makombora Iran, Trump akionya Tehran

Marekani imerusha mabomu kwenye maeneo ya Vinu vya Nyuklia vya Iran yanavyojumuisha Fordo na kuharibu kabisa maeneo hayo hatua ambayo huenda ikachangia vita zaidi ya kimataifa.
Rais wa Marekani Donald Trump alisema maeneo hayo yanayojumuisha Fordo, yalipigwa na makombora ya jeshi la Marekani huku Marekani ikijiunga na mashambulio ya Israel dhidi ya mpango wa Nyuklia wa Tehran.
Katika hatuba yake vya vyombo vya habari, Rais Trump alisema kwamba ni lazima Iran isitishe vita na kukumbatia amani iwapo wanataka vinu vyao vya Nyuklia kutorushiwa makombora.

Picha kwa hisani
“Tayari tumevuruga na kuharibu vinu vya Nyuklia vya Iran na bado tutaendelea kurusha makombora ya kasi zaidi na kuharibu vinu vyote vya Nyuklia vya Iran iwapo makao ya Tehran hayatasalimu amri”, alisema Rais Trump katika hotuba yake.
Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya nje wa Iran Seyed Abbas Araghchi alilaani vikali shambulizi la Marekani na kusema kwamba ni shambulizi la kuchukiza na kwamba Tehran ina njia zote za kutetea uhuru wake.
“Matukio ya asubuhi ya leo ni ya kuchukiza na yatakuwa na matokeo ya milele. Kila Mwanachama wa Umoja wa Mataifa ni lazima ashtushwe na tabia hii hatari sana, isiyo ya kisheria bali ni tabia ya kihalifu,” alisema Seyed.
Seyed aliongeza kwamba Marekani ilifanya ukiukaji mkubwa wa Katiba ya Umoja wa Mataifa kama Mwanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi