Sports

Chelsea Yathibitisha Kunasa Joao Pedro

Published

on

Kilabu ya Chelsea imethibitisha kumsajili mshambulizi wa kilabu ya Brighton and Hove Albion FC Joao Pedro raia wa Brazil kwa pauni milioni 60.

Mchezaji huyo amesafiri tayari Marekani baada ya kukamilisha vipimo vya kimatibabu mjini london NA kutia wino mkataba wa miaka mitano na The Blues.

Nyota huyo anakua sajili wa tatu kwa Chelsea ambao mpaka sasa wametumia zaidi ya pauni milioni 200 katika kusajili wachezaji.

Pedro mwenye umri wa miaka 23 sasa yuko njia nyeupe kuwakilisha The Blues kwenye mechi ya robo fainali Kombe la Dunia baina ya vilabu nchini Marekani dhidi ya Fluminese ya Brazil.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version