Wafanyabiashara wa soko la kwa Charo wa mae mjini kilifi kaunti ya Kilifi, wanaitaka serikali ya kaunti kuwaondoa wachuuzi wanaoendeleza biashara zao nje ya Soko hilo.
Wakiongozwa na Florence Kazungu, wafanyibiashara hao wanasema kuwa biashara imepungua kwani wateja wengi wananunua bidhaa nje ya soko hali inayofanya mapato yao kupungua.
Wamesema kuwa licha ya wao kulipa ushuru katika soko hilo, bidhaa zao zinasalia sokoni kutokana uhaba wa wateja hali inayowasababishia hasara kwani bidhaa nyingi huharibika.
Hata hivyo wanaitaka serikali ya kaunti kuingilia kati suala hili na kuwaondoa wachuuzi hao.
“Biashara iko chini wateja hawaingii sokoni kwa sababu wananunua bidhaa hapo nje ya soko hali inayotufanya tunasalia na bidhaa zetu hadi zinaharibika ili hali tunalipa ushuru, serikali inafaa iwatoe wachuuzi hao ili sisi nasi tuweze kupata riziki ya kila siku”. alisema Florence.
Taarifa ya Pauline Mwango
