News

Anselm: Viongozi wanajukumu la kutimiza ahadi kwa wananchi

Published

on

Kaimu Spika wa bunge la kaunti ya Taita Taveta Anselm Mwadime ametoa wito kwa viongozi wa kaunti hiyo kuwajibika vilivyo katika kutetea maslahi ya wakaazi wa kaunti hiyo kama suala la usalama wao ambao umedorora mno.

Mwadime alisema wananchi wa kaunti hiyo wanaendelea kuhangaika na hakuna mikakati ambayo imewekwa na viongozi wa kaunti ili kupatikane mwafaka.

Mwadime alisema usalama wa wenyeji unapaswa kupewa kipaumbele hasa kwa wahudumu wa bodaboda ambao wamekuwa wakiuliwa katika hali tatanisha.

Wakati huo huo Mwadime alisema ni lazima mauaji ya wahudumu hao wa bodaboda yadhibitiwe vilivyo na wahusika wakabiliwe kisheria na kufikia sasa ni takribani visa 8 vya wahudumu hao wa bodaboda ambao wameuwawa katika kipindi cha mwaka mmoja huku pipiki zao zikiibiwa.

Haya yalijiri katika hafla ya mazishi ya Darmian Legha aliyeuawa kinyama na abiria wawili juma lililopita katika eneo la chuo kikuu Cha Taita na kutoweka na pikipiki yake.

Taarifa ya Janet Mumbi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version