National News

Mahakama Kuu ya Malindi Yahairisha Kesi ya Ulaghai

Published

on

Mahakama kuu mjini Malindi kaunti ya Kilifi imeahirisha kwa mara ya mwisho uamuzi wa kesi ya madai ya ulaghai wa fedha unaodaiwa kutekelezwa na Kenneth Njoroge Maina kwa mtalii Garallin Chiara.

Hakimu mkaazi wa Mahakama hiyo, Nkurrunah Namunyak amesema uamuzi wa kesi hiyo ulikuwa tayari ila mshtakiwa ameshindwa kufika Mahakamani kwa mara sita mfululizo kwa madai ya changamoto za kiafya.

Kulingana na stakabadhi za kesi hiyo, Maina anadaiwa kumlaghai Chiara shilingi 124,800 za kusimamia huduma za usafiri wa mtalii huyo kutoka Malindi hadi mbuga ya wanyama ya Tsavo na kukosa kutimiza ahadi yake.

Kupitia Wakili wa Maina, hapo awali alieleza Mahakama kwamba alikuwa amepata asilimia 70 ya fedha za mlalamishi na akataka kumrudishia Chiara fedha zake japo Mahakama hiyo ilidai kwamba wakili wa mshtakiwa alishindwa kuieleza Mahakama kuhusu ugonjwa wa mshtakiwa.

Uamuzi wa kesi hiyo unatarajiwa kutolewa mnamo siku ya Jumatatu tarehe 17 mwezi Machi mwaka huu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version