National News

Kanja Awataka Maafisa wa Usalama Kutekeleza Majukumu Yao

Published

on

Inspekta jenerali wa polisi nchini Douglas Kanja, amewataka maafisa wa usalama nchini kutekeleza majukumu yao kikamilifu kwa kuzingatia sheria za nchi.

Kanja amesema ni sharti maafisa wa usalama kuwahudumia wananchi ipasavyo, akionya kwamba watakaokaidi agizo hilo watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Akizungumza katika kaunti ya Mombasa Kanja amewataka wakenya kushirikiana na maafisa wa polisi katika kukabiliana na utovu wa usalama.

“katika muongozo wangu nimesema kwamba maafisa wa polisi kufanya kazi kwa kuzingatia sheria ili kuimarisha usalama mashinani”, Kanja.

Kwa upande wake Kamanda wa polisi eneo la Pwani Ali Nuno, wameahidi kushirikiana na wananchi kuhakikisha usalama unaimarika.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version