News

Wanaharakati Waitaka Serikali Kuongeza Muda wa Kuvifanyia Vipimo vya DNA Familia Zilizopoteza Zilizofiwa Shakahola

Published

on

Wanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu katika eneo bunge la Malindi na Magarini kaunti ya Kilifi wanaitaka serikali ya kitaifa kuongeza muda wa kuvifanyia vipimo vinasaba yani DNA za familia zilizopoteza wapendwa wao katika msitu wa Shakahola.

Wakiongozwa na Thomas Karisa, Wanaharakati hao wamesema miili mingi iliyofukuliwa katika makaburi ya msitu wa Shakahola haijatambuliwa hali ambayo imeziacha familia zilizowapoteza wapendwa wao kusalia katika njia panda.

Karisa ameitaka serikali kuikabidhi miili iliyotambuliwa kwa familia husika kwa ajili ya maandalizi ya mazishi na pia kuchukua jukumu la kuizika miili ambayo haitatambulika hata baada ya kukamilika kwa muda wa uchunguzi.

Kwa upande wake Stephen Mwiti ambaye alipoteza watoto wake 5 katika msitu wa Shakahola amesema amepoteza matumaini ya kuipata miili ya wanawe licha ya kufanyiwa vipimo vya DNA tangu mwaka uliopita.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version