News

Waziri Joho na Mvurya waonya wanyakuzi wa ardhi.

Published

on

Waziri wa madini na uchumi wa bahari nchini Ali Hassan Joho alisema serikali haitaruhusu tena wakaazi kufurushwa katika ardhi wanayoishi.

Akizungumza katika maeneo ya Mzambarauni mjini Mtwapa eneo bunge la Kilifi Kusini kaunti ya Kilifi, Joho alionya kwamba mabwenyenye wenye hulka ya kufurusha wananchi kwenye ardhi za umma kamwe hawataruhusiwa.

Joho alisema wananchi hawafai kuhangaishwa kwenye ardhi zao huku akiwatahadharisha maafisa wa serikali dhidi ya kushirikiana na mabwenyenye kuhangaisha raia kwenye ardhi zao.

Hii ni baada ya kuibuka malalamishi ya mabwenyenye kutaka kuwafurusha wakaazi wa Utange Kaunti ya Mombasa.

Kwa upande wake Waziri wa michezo na Sanaa nchini Salim Mvurya alidokeza kuwa serikali inapanga kununua mashamba ambayo hayatumiki ili kuyakabidhi ya wananchi.

Taarifa ya Joseph Jira

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version