Business
Wavuvi wa Kilifi wanalalamikia ukiukaji wa sheria za kuvua samaki
Wavuvi kutoka eneo la Old Ferry wanadai kuna baadhi ya wavuvi ambao wanatumia nyavu ambazo zilipigwa marufuku.
Kulingana na wavuvi, Nyavu hizo zinavua hadi samaki wadogo na kuharibu maeneo ya samaki ya kuzaana hali ambayo inasababisha kupungua kwa idadi ya samaki baharini.
Wakiongozwa na James Kahindi, Wavuvi hao walisema sekta ya uvuvi imedorora kutokana na upungufu wa samaki kwani vifaa wanavyotumia ni hafifu na haviwezi kuvua katika maji makuu.
Wakizungumza na Coco Fm, Wavuvi hao walitoa wito kwa serikali ya kaunti ya Kilifi kuwawezesha wavuvi kifedha na hata kuwapa vifaa vya kisasa ili kuweza kuvua samaki kwenye maji makuu
Taarifa ya Pauline Mwango