Connect with us

Business

Wavuvi wa Kilifi wanalalamikia ukiukaji wa sheria za kuvua samaki

Published

on

Wavuvi kutoka eneo la Old Ferry wanadai kuna baadhi ya wavuvi ambao wanatumia nyavu ambazo zilipigwa marufuku.

Kulingana na wavuvi, Nyavu hizo zinavua hadi samaki wadogo na kuharibu maeneo ya samaki ya kuzaana hali ambayo inasababisha kupungua kwa idadi ya samaki baharini.

Wakiongozwa na James Kahindi, Wavuvi hao walisema sekta ya uvuvi imedorora kutokana na upungufu wa samaki kwani vifaa wanavyotumia ni hafifu na haviwezi kuvua katika maji makuu.

Wakizungumza na Coco Fm, Wavuvi hao walitoa wito kwa serikali ya kaunti ya Kilifi kuwawezesha wavuvi kifedha na hata kuwapa vifaa vya kisasa ili kuweza kuvua samaki kwenye maji makuu

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Wahudumu wa Uchukuzi Kilifi Walia na Kupanda kwa Bei ya Mafuta

Published

on

Siku moja baada ya mamlaka ya udhibiti wa kawi nchini, EPPRA kutangaza kupandishwa kwa bei ya mafuta, sekta ya uchukuzi katika kaunti ya Kilifi inaelezea hofu ya kuathirika kwa biashara zao.

Wahudumu wa tuktuk,teksi, bodaboda na magari ya usafiri wa umma hapa mjini Kilifi wanasema kupanda kwa bei ya petrol na diseli kutaathiri pakubwa sekta hiyo ya uchukuzi.

Sasa wanasema kuwa watalazimika kuongeza nauli kwa abiria kutokana na gharama ya mafuta.

Ni hali ambayo imeathiri wakaazi ambao wanatarajiwa kutumia vyombo hivyo vya usafiri wakisema kuwa watalazimika kutembea kwa mguu kwa safari fupi fupi katika utekelezaji wa shughuli zao za kawaida.

Hatahivyo wametoa wito kwa serikali kuhakikisha kuwa inaingilia kati ili kuona kwamba bei za mafuta zinadhibitiwa.

Haya yamejiri huku lita moja ya mafuta aina ya petrol kaunti ya KIlifi ikiuzwa kwa shilingi 183.88 huku diseli ikiuzwa kwa shilingi 169.16 kila lita.
Lita moja ya mafuta ya taa inauzwa kwa shilingi 153.29.

Continue Reading

Business

Uhusiano wa Kibiashara kati ya Kenya na Ufaransa Waonyesha Ukuaji Chanya

Published

on

Takwimu za kibiashara kati ya kenya na ufaransa katika kipindi cha miezi mitatu ya mwisho wa mwaka 2024 zinaonyesha kuwa ufaransa ilileta humu nchini bidhaa za thamani ya shilingi bilioni 6.5 na kuagiza bidhaa za thamani ya shilingi bilioni 5.7 kutoka humu nchini hali iliyoleta uwiano bora wa kibiashara kati ya nchi hizi mbili.

Nchi hiyo sasa inalenga kuimarisha zaidi uhusiano wake na kenya ambapo kenya imewaalika waekezaji zaidi kutoka nchini ufaransa kuekeza katika sekta kadhaa za kenya.

Waziri mwenye mamlaka makuu Msalia Mdavadi anasema ufaransa inalenga sekta za kawi, miundomsingi na tekinolojia ili kuongeza biashara kati yake na kenya.

Continue Reading

Trending