Business

Wavuvi Old Ferry Wageukia Biashara ya Mahindi Kutokana na Uhaba wa Samaki

Published

on

Baadhi ya wavuvi kutoka eneo la old ferry kaunti ya kilifi wamegeukia biashara ya kuchoma mahindi machanga kutokana na kutoweza kuingia baharini.

Wavuvi hao wamesema kuwa msimu huu wa kusi hakuna samaki hali ambayo imefanya kuingilia biashara ya kuchoma mahindi ili kujiendeleza kimaisha.

Kulingana na wavuvi kutokana na uhaba wa vifaa vya kisasa hawawezi kuingia katika maji marefu ili kuvua samaki.

Hata hivyo wameitaka serikali kuwawezesha na vifaa vya kisasa ili waweze kuvua katika maji marefu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version