Entertainment
Wakili George Kithi na Mbosso Khan Waanzisha Ushirikiano wa Kimkakati kuinua Muziki wa Africa Mashariki
Wakili na mwanasiasa maarufu kutoka Kilifi, George Kithi, ameweka wazi azma yake ya kuendelea kukuza sekta ya muziki na ubunifu katika ukanda wa Pwani ya Kenya kwa njia za kimkakati na kimataifa.
Wakili Kithi aliyasema haya Jijini Dar es salaam Tanzania alipokutana na kufanya mazungumzo na Mwanamuziki nyota wa Bongo flavor, Mbosso Khan, katika mazungumzo yaliyolenga kuleta mageuzi ya kweli katika Sekta ya muziki wa Pwani na Kenya kwa ujumla.
“Nilifanya kikao chenye mafanikio na msanii maarufu kutoka Tanzania, Mbosso Khan, jijini Dar es Salaam, ambapo tulijadili mbinu za kimkakati katika kuboresha muziki na kukuza wasanii hususan kutoka Kaunti ya Kilifi na eneo zima la Pwani.,” Kithi alisema.
Mkutano huu ni hatua Moja wapo ya kuendeleza uhusiano kati ya Kiongozi huyo na Mwanamuziki Mbosso baada ya ziara ya Mwanamuziki huyo Mjini Kilifi mnamo Desemba 31, 2023, ilitia fora na kuweka Msingi mahusiano bora.
Ziara ya Mbosso mjini Kilifi ilizua gumzo Kwa jinsi ilivyoshabikiwa kufuatia show yake ya kukata na shoka katika eneo la Old Fery Kilifi, na kuwavutia maelfu ya mashabiki.
Tukio hilo liliangazia kiwango cha hamasa na kiu ya burudani ambayo Pwani inayo na huenda ndicho Kithi anataka kuendeleza kwa vitendo.
Miongoni mwa mambo wanayolengwa katika usjirikiano huu pia ni kuleta mshikamano na ushirikiano wa karibu baina ya wasanii wa Africa Mashariki Kwa lengo ya kukuza sekta na muziki Kwa kutumia teknolojia ya kisasa, vifaa bora, na ubadilishanaji wa maarifa kutoka pande zote mbili za mipaka.
Zaidi ya hayo, walitathmini njia za kuwasaidia wasanii kibiashara kwa kuwapatia mafunzo kuhusu jinsi ya kutumia teknolojia kupata mapato kupitia majukwaa mbali mbali ya kidijitali mfano mapato ya muziki kupitia mtandaoni (streaming royalties), uuzaji wa maudhui (content monetization), ushirikiano na chapa mbalimbali (brand partnerships), pamoja na mbinu za kujenga hadhira kupitia mitandao ya kijamii. Lengo kuu likiwa ni kuhakikisha kuwa kipaji kinaweza kubadilishwa kuwa taaluma, na muziki kuwa chanzo halisi cha mapato.
Kwa mujibu wa Kithi, mafunzo haya yatasaidia sana kubadilisha fikra za muziki kuwa kipaji tu, hadi kuwa chanzo cha mapato na ajirankwa vijana wa Pwani.
Huenda hii ikawa hatua kubwa kuelekea kuinua uchumi wa kijamii kupitia sekta ya ubunifu.
“Maarifa katika eneo hili yanaweza kubadilisha ari kuwa taaluma na kipaji kuwa chanzo cha mapato,” alisema Kithi.
“Tumejikita katika kukuza vipaji, kujenga ushirikiano, na kuunda fursa zitakazoinua vijana wetu na kuiweka kanda yetu kwenye ramani ya dunia” aliongezea.
George Kithi ametangaza kuwa kuna mengine mengi yanakuja, ikiwa ni pamoja na miradi mipya ya ushirikiano, mafunzo ya ubunifu, na kuibua vipaji vijijini.