Sports

Rasmi Mshambulizi wa Uswidi Alexander Sasa ni Mali ya Liverpool

Published

on

Kilabu ya Liverpool wakubaliana kumsajili mshambuliaji wa Uswidi Alexander Isak kutoka Newcastle United

Liverpool wamekubaliana kumsajili mshambuliaji wa Uswidi Alexander Isak kutoka Newcastle United kwa mkataba wa muda mrefu kwa ada ya rekodi ya Uingereza inayokadiriwa kufikia pauni milioni 130 ($175 milioni), vyombo vya habari vya Sky Sports News na The Athletic viliripoti Jumapili.

Mazungumzo ya muda mrefu kuhusu dili hilo yamekuwa yakitawala dirisha la usajili la Ligi Kuu ya England, ambalo linahitimishwa Jumatatu, huku ofa ya awali ya Liverpool ya pauni milioni 110 kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 ikikataliwa mapema Agosti.

Mchezaji huyo amepasi vipimo vya kimatibabu na anatarajiwa kumwaga wino mkataba wa miaka mitano na The Reds.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version