News

Rais Ruto: Mradi wa ujenzi wa nyumba za bei nafuu utaendelea

Published

on

Rais William Ruto amesema lengo kuu la serikali ya Kenya kwanza ni kuhakikisha wakenya wananufaika kimaendeleo na wala sio siasa za vurugu na migawanyiko.

Rais Ruto alisema mpango wa kujenga nyumba za bei nafuu katika maeneo mbalimbali nchini utaendelea ili kuhakikisha wakenya wanamudu gharama ya maisha kwani watakuwa na nafasi nzuri kwenye makaazi bora.

Akizungumza jijini Nairobi, Rais Ruto alisema viongozi wengi wamebali kushirikiana na serikali akiwemo Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga ili kuhakikisha wakenya wanafaidi na raslimali zao.

Kiongozi wa nchi, aliweka wazi kwamba atahakikisha miradi yote ya maendeleo nchini inatekelezwa kupitia ushirikiano wa viongozi na wananchi, huku akiwakosoa wale wanajaribu kurudisha nyuma juhudi za maendeleo.

“Tuko na mpango wa kujenga nyumba za bei nafuu kwani wananchi wetu, watu wengi wanaisha katika nyumba duni na alisema hii maneno tutafanya hata wale wengine waongee maneno mengi mimi nitahakikisha natekeleza jukumu langu”, alisema rais Ruto.

Wakati uo huo aliahidi wakenya kwamba serikali itaendelea na mpango wake wa bima ya afya ya jamii SHA, ili kuwawezesha wananchi wa kipato cha chini wanapata matibabu bila ya kuanganishwa huku akiwarai wakenya kujisajili na SHA.

“Kila mkenya ni lazima apate matibabu kwa gharama ya chini ndio tunasema ni vuzuri wakenya wajisajili katika SHA na tayari wale ambao waliweza kujisajili wameona manufaa ya SHA na kweli tumesajili watu zaidi ya milioni 20”, aliongeza Rais.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version