News

Lagat, ahojiwa na IPOA kuhusu kifo cha Ojwang’

Published

on

Naibu Inspekta jenerali wa polisi Eliud Lagat aliandikisha taarifa kwa maafisa wa uchunguzi wa Mamlaka ya kuchunguza utendakazi wa maafisa wa polisi nchini IPOA.

Lagat, aliandikisha taarifa hiyo kuhusu mauaji ya mwanablogu Albert Ojwang’, baada ya kuagizwa na IPOA kufika mbele ya maafisa hao kuhojiwa kwani alikuwa kati ya maafisa waliohusishwa na kifo cha Ojwang’. 

Lagat ambaye alikuwa mlalamishi kwenye kesi hiyo ambayo inasemekana kwamba Marehemu Ojwang’ alituhumiwa kwa kuchapisha taarifa zisizo za ukweli kuhusu Lagat katika mitandao ya kijamii.

Kulingana na taarifa kutoka IPOA, Lagat alihojiwa kwa masaa kadhaa na maafisa wa uchunguzi wa kesi hiyo sawa na kuandikisha taarifa kuhusu kile anachokifahamu kuhusu kukamatwa na kusafirikishwa hadi katika kituo cha polisi cha Central jijini Nairobi.

Ripoti kuhusu kuhojiwa kwa Lagat japo haijawekwa wazi masuala ya ndani kuhusu mahojiano hayo, kuna tetesi kwamba afisa huyo wa polisi aliweka wazi kuhusiana na kukamatwa kwa Albert Ojwang’ kutoka pamoja na kilichojiri katika kituo cha polisi cha Central jijini Nairobi kabla ya kifo cha Ojwang’.

Lagat hata hivyo anaongeza idadi ya watu ambao tayari walihojiwa kuhusiana na mauaji ya Ojwang’ na kwamba kufikia sasa tayari maafisa 20 walifika mbele ya Mamlaka ya IPOA kuandikisha taarifa.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version