News

Hofu ya Ongezeko la HIV

Published

on

Shirika la umoja wa mataifa la kupambana na virusi vya UKIMWI, UNAIDS, limesema huenda kukawa na maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi milioni 6 na vifo milioni 4 vinavyohusiana na ukimwi kufikia mwaka 2029.

Hii ni kutokana na kupunguzwa kwa fedha za misaada ya kiafya kutoka Shirika la Marekani, USAIDS.

Kulingana na takwimu, taifa la Afrika kusini ndio taifa lenye idadi kubwa zaidi ya watu wanaoishi na virusi vya ukimwi ulimwenguni lakini pia nchi inayoongoza katika utafiti wa virusi vya ukimwi ulimwenguni.

Miongoni mwa mataifa mengine, Afrika kusini pia imekuwa nchi ambayo pia ilikuwa ni mpokeaji mkubwa wa fedha za UKIMWI kutoka Marekani hadi Machi mwaka huu, wakati utawala wa Rais Trump ulipotangaza kufungwa kwa Shirika la USAID.

Mwezi uliopita vyuo vikuu vya juu vya Afrika Kusini viliomba serikali madola ya mamilioni ili kuendelea na utafiti huu ambao baadhi umesitishwa kwa sababu ya kupunguzwa kwa fedha na Marekani.

Pesa hii ilisaidia nchi hiyo kupunguza kiwango chake cha maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi kwa zaidi ya asilimia 60 tangu kilele chake mnamo 2000.

Siku ya Jumatano tarehe 9 Julai 2025, serikali ya Afrika Kusini na wafadhili wa kimataifa waliahidi karibu dola milioni 54 ili kukabili palipo na mapungufu.

Mwaka jana Marekani ilitumia mara nane ya kiwango hicho kwa ufadhili wa Virusi Vya Ukimwi Afrika Kusini kiwango hiki hakitatosha kutimiza hitaji lililopo.

Taarifa ya Hamis Kombe

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version