News

Dkt. Nzai, awahimiza vijana kujisajili kwa mpango wa elimu kwa wote

Published

on

Kama njia mojawapo ya kuimarisha vijana wa Pwani kupitia elimu, Jumuiya ya kaunti za Pwani imeanzisha mpango wa elimu kwa wote unaotoa elimu ya juu kupitia mtandao.

Mkurugenzi wa Jumuiya ya kaunti za Pwani, Dkt. Emmanuel Nzai alisema wanalenga vijana elfu tano kupitia mpango huo huku idadi lengwa ya vijana wa kaunti ya Kilifi ikiwa 700.

Dkt. Nzai alitoa wito kwa vijana kujisajili kwenye mpango huo ikizingatiwa kwamba ni vijana 25 pekee katika kaunti ya Kilifi ambao tayari wamejisajili kwenye mpango huo.

Dkt. Nzai alidokeza kwamba wanashirikiana na taasisi ya kimataifa ya Regeneysis kufanikisha mpango huo.

Kwa upande wake Waziri wa Elimu kaunti ya Kilifi Felkin Kaingu alisema kupitia wafadhili mbalimbali watahakikisha kuwa vijana watakaojisajili kwenye mpango huo wanafadhiliwa kuendeleza masomo yao.

Hata hivyo vijana ambao tayari walinufaika na mpango huo walisisitiza haja ya hamasa zaidi kutolewa kwa vijana hasa wa mashinani ili wapate kujua kuhusu mpango huo wa elimu kwa wote.

Taarifa ya Hamis Kombe

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version