Connect with us

News

Kilabu Ya Barcelona Yakabwa Koo UEFA

Published

on

Miamba wa Uhispania kilabu ya Barcelona kina kibarua kigumu mechi ya mkondo wa pili nchini Italia baada ya kutoka sare ya magoli 3-3 dhidi ya Intermilan mechi ya mkondo wa kwanza ugani Estadio Olympic St.luis Companys siku ya jumatano.

Mshambulizi wa Ufaransa Marcus Thuram alihitaji dakika moja pekee kuwaweka uongozini vijana wa kocha Simeone Inzaghi baada ya pasi murwa kutoka kwa beki Denzil Dumfries ambaye aliongeza la pili dakika 20 badaye na kufanya mambo kuwa magoli 2-0

Hata hivyo Barcelona walikua na jambo lao wakipiga comeback ya haraka haraka kupitia winga matata tineja Lamine Yamal kunako dakika ya 24 kabla ya Ferran Torres kuweka mambo sawa dakika ya 38.

Hata hivyo licha ya kuchukua uongozi tena kupitia goli lake Denzel Dumfries dakika ya 63 The Catalans walihitaji dakika moja kusawazisha kupitia goli la kujifunga la kipa Yan Sommer baada ya mkwaju kali ilitumwa kimyani na winga wa Brazil Raphinha kunako dakika ya 64.

Mshambulizi Lamine Yamal akiwa na umri wa miaka 17 alikua anashiriki mechi yake ya 100 tangu anze kuchezea vinara hao wa Laliga.

Mechi ya mkondo wa pili itapigwa siku ya jumanne ugani San siro ambapo yeyote ana uwezo wa kupiga hatua kwenye nusu fainali hiyo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Aisha Jumwa akosolewa kutokana na matamshi yake

Published

on

Jopo la ushauri la viongozi na maimamu wa Takaungu wadi ya Mnarani kaunti ya Kilifi limeeleza kusikitishwa na kauli zilizotolewa na Aisha Jumwa kuhusiana na tukio la mauaji na maziko ya kijana mmoja eneo hilo lililomtaja kama Zakariyah Kirao Charo.

Likizungumza na vyombo vya habari, jopo hilo likiongozwa na sheikh Mahadh Ali wa msikiti Maryam limemkosoa Jumwa kwa kile lilichosema ameuhujumu uislamu kutokana na kauli alizotoa kwenye mtandao wake wa kijamii wa tiktok kuhusiana na mazishi ya kijana huyo.

Sheikh Mahadh amesema Jumwa alidai kuwa familia ya marehemu haikuhusishwa ilhali walichukua wajibu wa kuihusisha familia kabla ya hatua zozote kuchukuliwa ila wanafamilia wenyewe hawakuonyesha ushirikiano akieleza kuwa jopo hilo pia liligadhabishwa na kauli za Jumwa kuhusiana na namna mchakato mzima wa mazishi ulivyofanywa.

Akiunga mkono kauli hiyo Ustadh Mohamed Khamis amesema kwenye mkao huo kuwa amekuwa akipokea vitisho kutoka kwa Jumwa tangia mtafuruku huo ulipoanza akisisitiza haja ya swala hilo kutotumika kwa namna ya kuchochea wanajamii waislamu na wasio kuwa waislamu katika eneo hilo la Takaungu.

Aisha Jumwa /Picha kwa hisani

Ustadh Mohamed pia amekinzana na kauli kuwa marehemu alisilimishwa akiwa na matatizo ya kiakili akisema ni sharti swala hilo lisiingiziwe siasa.

Continue Reading

News

Viongozi wa Kilifi Wapinga Uekezaji wa Mradi wa Kawi ya Nuklia

Published

on

By

Wizara ya Kawi nchini imefanya kikao cha mazungumzo na uongozi wa kaunti ya Kilifi, pamoja na wabunge na Wasimamizi wa Shirika la NUPEA kuhusu uekezaji wa mradi wa uzalishaji kawi ya Nuklia katika kijiji cha Uyombo wadi ya Matsangoni katika eneo bunge la Kilifi Kazkazini katika kaunti ya Kilifi.

Akizungumza na Wanahabari baada ya kikao hicho mjini Kilifi, Waziri wa Kawi nchini Opiyo Wandayi amesema japo viongozi wa kaunti ya Kilifi pamoja na wananchi hawajaridhishwa na uekezaji wa mradi huo, mazungumzo kuhusu mradi huo bado yataendelea ili kuibuka na mwafaka kwani utasaidia pakubwa katika uzalishaji kawi.

Kwa upande wake Gavana wa Kilifi Gedion Mung’aro amesema msimamo wa serikali ya kaunti ya Kilifi pamoja na wananchi bado uko pale pale wa kuendelea kupinga uekezaji wa mradi huo wa mabilioni ya pesa, akisema utafiti uliofanywa umebaini kwamba mradi huo unaathari kubwa kwa wananchi.

Hata hivyo Mbunge wa Kilifi Kazkazini Owen Baya amesema kama viongozi kutoka kaunti ya Kilifi hawako tayari kupokea mradi huo wa uzalishaji kawi ya Nuklia, akisema changamoto nyingi bado hazitatuliwa katika mradi huo ambazo ni athari kwa wananchi.

Kikao hicho hata hivyo kimehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mbunge wa Malindi Amina Mnyazi, Mbunge wa Kaloleni Paul Katana, Mbunge wa Kilifi Kusini Ken Chonga, Mbunge wa Ganze Kenneth Tungule, Katibu katika Wizara ya masuala ya vijana na michezo nchini Fikirini Jacobs miongoni mwa viongozi wengine.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.