News
Chonga, Akemea Idara ya Polisi kwa Kukiuka Sheria za Ardhi
Mbunge wa Kilifi kusini Ken Chonga ameikemea Idara ya Polisi kwa kukiuka sheria na kushirikiana na mabwenyenye kuwahangaisha wakaazi kwenye ardhi zao.
Chonga amekariri kwamba kutokana na ulegevu unaoshuhudiwa kwenye idara ya polisi, baadhi ya mabwenyenye wamekuwa wakiendeleza tabia ya kuwatumia polisi vibaya ili kuwanyanyasa wakaazi kuhusu suala la ardhi.
Aidha ameeleza kuchukizwa na hulka hiyo ya kuwafurusha wakaazi kwenye ardhi zao kwa madai ya kuwa wamiliki halali wa ardhi hizo, akisema wengi wa wakaazi wameishi kwenye ardhi hizo tangu jadi.
Wakati huo huo amesema tayari analenga kufanya mazungumzo na wakuu wa idara ya polisi nchini sawa na Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro ili kuibuka na suluhu kuhusu suala hilo.