News

Tahadhari Yatolewa Kuhusu Mvua Kubwa

Published

on

Idara ya utabiri wa hali ya hewa nchini imetoa tahadhari kwa wakenya kuhusu mvua kubwa itakayonyesha katika maeneo mbalimbali ya nchi kwa kipindi cha siku saba.

Mkurugenzi wa idara ya hali ya hewa nchini, Dkt David Gikungu, amesema mvua hiyo itakayoambatana na ngurumo za radi inatarajiwa wakati wa alasiri na usiku, huku baadhi ya maeneo yakitarajiwa kupata mvua chache asubuhi kabla ya hali ya jua kuchomoza kwa muda mfupi.

Idara hiyo imesema viwango vya joto usiku katika maeneo haya vitashuka hadi chini ya nyuzi joto 9, hali inayoweza kuathiri watoto, wazee, na wagonjwa.

Kaunti za Siaya, Kisumu, Homa Bay, Migori, Kisii, Nyamira, Trans Nzoia, Baringo, Uasin Gishu, Elgeyo-Marakwet, Nandi, Nakuru, Narok, Kericho, Bomet, Kakamega, Vihiga, Bungoma, Busia, na Pokot Magharibi pia zimeorodhesha kati ya ya maeneo yanayotarajiwa kupokea mvua nyingi.

Hali kama hiyo inatarajiwa katika kaunti za Kitui, Makueni, Machakos, Kajiado, Taita Taveta, na sehemu za Tana River, ambako asubuhi kutakuwa na mawingu na mvua nyepesi kabla ya hali ya mvua kubwa kuanza alasiri na kuendelea hadi usiku.

Wakati mvua ikinyesha maeneo mengi ya kaunti za Mombasa, Kilifi, Lamu, Kwale, Marsabit, Mandera, Wajir, Garissa, na Isiolo yametabiriwa kupata joto nyakati za mchana hadi kufikia nyuzi joto 33.

Wataalamu wa hali ya hewa wamewahimiza wananchi kuwa waangalifu na kufuata ushauri wa serikali, hasa wale wanaoishi maeneo yenye historia ya mafuriko, maporomoko ya ardhi, na miundombinu dhaifu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version