National News

Famau: Maeneo ya Mijini Yameathirika Zaidi na Mihadarati

Published

on

Mwanaharakati wa kupambana na Mihadarati katika ukanda wa Pwani Famau Mohammed Famau amesema maeneo ya mijini yameoathirika zaidi na utumizi wa mihadarati ikilinganishwa na maeneo ya mashinani.

Famau amesema utumizi wa mihadarati umeathiri pakubwa vijana, akieleza kusikitishwa na swala hilo kwani vijana wenye umri mdogo tayari ni waraibu wa mihadarati.

Mwanaharakati huyo amesema kwamba serikali ina wajibu mkubwa wa kuimarisha vita dhidi ya mihadarati kupitia vitengo husika ili kuwanasua vijana wanaopotoka kila uchao kupitia utumizi wa dawa za kulevya.

Wakati huo huo amewarai wazazi kuwa waangalifu na watoto wao kwa kuhakikisha wanafuatilia mienendo yao ili kuwaepusha na utumizi wa Mihadarati, uhalifu na mimba za mapema.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version