Klabu ya wanawake mchezo wa Voliboli wanabenki (KCB) walitoka nyuma na kuwashinda wapinzani wao na mabingwa, Kenya Pipeline, kwa seti 3-1 katika pambano la nusu fainali na kujihakikishia nafasi ya kucheza fainali ya Mashindano ya Klabu Bingwa ya Mpira wa Wavu ya Wanawake Afrika (CAVB) jijini Cairo.
Mabenki hao walianza polepole, wakipoteza seti ya kwanza 25-16 huku Pipeline wakitawala mchezo katika hatua za mwanzo kwenye Uwanja wa Michezo wa Al Ahly.
Hata hivyo, KCB walirejea kwa nguvu, wakijipanga upya kwa ulinzi imara, mapokezi bora na mashambulizi makali yaliyoongozwa na Marline Terry Tata na Esther Mutinda na kuchukua udhibiti wa mchezo. Walishinda seti tatu zilizofuata kwa alama 25-10, 25-15 na 25-19 na kukamilisha mgeuko wa kukumbukwa.
Ushindi huo unaifanya KCB kufika fainali yao ya kwanza tangu 2022, waliponyakua taji la bara, na pia ni kisasi baada ya kupoteza dhidi ya Pipeline katika mechi ya kuwania nafasi ya tatu mwaka 2023.
Kocha mkuu Japheth Munala aliisifu timu yake kwa ustahimilivu, akibainisha kuwa mabadiliko ya kimkakati baada ya seti ya kwanza yalikuwa ya kuamua.
āTulianza vibaya kwenye mapokezi ya mpira lakini ninafurahi tulijibu vizuri. Ilibidi tufanye marekebisho ya kimkakati baada ya seti ya kwanza na wachezaji walitekeleza mpango wetu kikamilifu na hilo likatusaidia kushinda mchezo,ā alisema.
KCB walikuwa wakitawala mashindano yote, wakipoteza seti yao ya kwanza ya kampeni hii katika nusu fainali hii baada ya kushinda raundi za awali kwa seti zote.
Sasa watakutana na aidha mshindi wa pili wa mwaka jana na wenyeji Al-Ahly au klabu ya Tunisia ya Carthage Volleyball Club katika fainali.
Klabu hiyo sasa itavaana na AL-Ahly ya Misri kwenye marudio ya fainali ya mwaka 2022 ambapo KCB walishinda seti 3-1.
