Usalama umeimarishwa kabla ya ziara ya Rais Ruto, Kilifi

Usalama umeimarishwa kabla ya ziara ya Rais Ruto, Kilifi

Serikali imesema usalama umeimarishwa katika kaunti ya Kilifi kabla ya ziara ya rais William Ruto juma lijalo katika halfa ya uzinduzi wa ujenzi wa uwanja wa kitaifa katika eneo la Tezo na miradi mingine zaidi ya 20 kaunti ya Kilifi.

Kamishna wa kaunti ya Kilifi David Wanyonyi na Katibu katika Idara ya ulinzi nchini Dkt Patrick Mariru, wamesema maafisa wa usalama wanashika doria katika kila sehemu ya kaunti ya Kilifi.

Akizungumza na Wanahabari baada ya ukaguzi wa matayarisho ya ujenzi wa uwanja wa Ronald Ngala katika eneo la Tezo kaunti ya Kilifi, Katibu katika Wizara ya ulinzi nchini Dkt Patrick Mariru amesema mipango na mikakati imeandaliwa.

Kamishna wa kaunti ya Kilifi David Wanyonyi amesema vitengo mbalimbali vya kiusalama vinashirikiana kuhakikisha visa vya utovu wa usalama vinakomeshwa ili kufanikisha shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Katika katika Wizara ya ulinzi Dkt Patrick Mariru afanya ukaguzi wa ujenzi wa uwanja wa Ronald Ngala, eneo la Tezo kaunti ya Kilifi

Wanyonyi alisisitiza kwamba vikundi vya kihalifu vitakabiliwa kwani maafisa hao wanashika doria pia katika miji mkuu ikiwemo Kilifi, Malindi, Watamu na Mtwapa huku onya kukomeshwa visa vya dhulma za kijinsia.

Kwa upande wake Kiongozi wa wengi katika bunge la kitaifa ambaye pia ni Mbunge wa Kilifi Kaskazini Owen Baya amesema ziara ya rais Ruto ni mafanikio makubwa kwa wakaazi wa Kilifi kwani zaidi ya miradi 20 itazinduliwa.