News
Ni Lazima Tushinde Paris Asema Arteta
Mkufunzi wa kilabu ya Arsenal Mikel Arteta angali na imani kwamba vijana wake watanyuka Psg ugenini na kufuzu kwenye fainali ya kilabu bingwa ulaya wiki ijayo mjini Paris.
Akizungumza baada ya The Gunners kukubali kichapo cha goli 1-0 mechi ya mkondo wa kwanza Arteta amedai kwamba mchezo huo walipoteza kutokana na vitu vichache vya kimbinu kipindi cha kwanza ambapo wapinzani wao waliwalemea kimbinu zaidi.
“Bado mechi haijaisha ni nusu tu,bado dakika zingine 90 mjini Paris na tunaenda kwa ajili ya kuvuna ushindi hakuna lingine,”Asema Arteta
Kwa mujibu wa mwalimu huyo wanahitaji kuwa katika ubora wao kuangusha Psg kwani wako na timu nzuri ila lengo lao linasalia pale pale kushinda na kufuzu kwenye fainali mwezi wa May 31.
“Ni lazima tuonyeshe uwezo wetu tokea dakika ya kwanza kwamba tunahitaji ushindi huo, nitafanyia mabadiliko ya kimbinu kikosi kabla ya kuelekea Paris na tuko tayari kupindua meza kule.”
Timu hiyo ililazwa goli 1-0 na miamba hao wa ufaransa kupitia goli lake Ousmane Dembele na sasa wanahitaji kushinda kwa zaidi ya magoli 2-0 mechi ya mkondo wa pili ugani Parc De Prince siku ya Jumatano wiki ijayo.