News

Mshukiwa wa Ugaidi Azuiliwa na Polisi Mombasa

Published

on

Maafisa wa Polisi mjini Mombasa wanamzuilia mwanamme mmoja baada ya kupatikana akiwa amebeba risasi na bidhaa zengine zinazokisiwa kuwa vilipuzi katika kivuko cha Feri cha Likoni.

Maafisa wa Polisi wamesema jamaa huyo anayefahamika kwa jina Shinali Amuna Komoro amekamatwa alipokuwa akivuka kivuko cha Feri cha Likoni akitokea kisiwani Mombasa.

Maafisa hao wamesema kabla ya mshukiwa huyo kukamatwa alikuwa ameabiri basi lililokuwa likivuka feri kuelekea upande wa Likoni na ametiwa nguvuni wakati maafisa wa usalama walipokuwa wakifanya ukaguzi katika kivuko hicho.

Akithibitisha kukamatwa kwake, Kamanda wa Polisi eneo la Likoni Geoffrey Ruheni amesema huenda mshukiwa alikuwa amepanga njama ya kutekeleza mashambulizi ya kigaidi ndani ya Feri.

Ruheni amesema mshukiwa huyo amekabidhiwa maafisa wa kupambana na ugaidi nchini ATPU kwa uchunguzi zaidi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version