Wakaazi wa Voi wapendekeza mbinu mpya za kulipa ada za maji

Wakaazi wa Voi wapendekeza mbinu mpya za kulipa ada za maji

Wakaazi wa kaunti ndogo ya Voi kaunti ya Taita Taveta wanapendekeza kampuni ya kusambaza maji mjini humo ya TAVEVO kubuni mbinu mpya ya kulipia ada ya maji kama ile ya kulipia umeme (Token) ili kumwezesha mteja wa maji kulipia kwa gharama anayoimudu.

Kulingana na wakaazi wengi wao wanakosa bidhaa hiyo muhimi ya maji kutokana na gharama ya juu wanayotozwa.

Walisema ikiwa kampuni hiyo ya kusambaza maji itakubali mapendekezo hayo huenda ikawapunguzia gharama ya kulipia maji.

‘’Kama tunaweza kuletewa Token wengi wetu tutaweza kulipa kwa gharama tunayoweza kumudu kuliko ile mita isome mpaka mwezi.Wengine wanashindiwa katikati wanakatiwa’’ alisema mkaazi

Wakati huo huo, wakaazi hao pia walishinikiza kampuni hiyo ya kusambaza maji ya Tavevo kubadilisha mita za zamani za maji na kuweka za plastic kama njia mojawapo ya kukabiliana na wizi wa mita hizo ambazo huwa zinang’olewa na kuuzwa kwa wanaonunua vyuma kuukuu.

‘’Sahizi tumekuwa na shida ya hizi mita, mita zang’olewa na sasa mimi nilikuwa napendekeza kama zinawezwa kubadilishwa na kuwekwe za plastiki kwa sababu inasemekana zinaibwa ziende ziuzwe kwa watu wa kununu scrap’’ aliongeza mkaazi.

Taarifa ya Janet Mumbi