Rais William Samoei Ruto amewaongaza wakenya kuadhimisha sherehe za kitaifa za 63 za Madaraka katika kaunti ya Wajir.
Hatua hii ni ya kihistoria kuwa kufanyika katika kaunti ya Wajir tangu taifa lijipatie uhuru kinyume na maeneo mengine ya taifa hili la Kenya.
Kaunti ya Wajir ni kati ya kaunti zinazopatika katika maeneo ya Kaskazini mwa Kenya na maeneo ambayo mara nyingi yamekuwa yakishuhudia misururu ya mashambulizi ya kigaidi, lakini kutoka na serikali kuchukua hatua ya kuimarisha usalama katika maeneo hayo, sasa wakaazi wa kaunti hizo wamaanza kushuhudia matunda miradi ya maendeleo.
Wakati wa halfa hiyo iliyohudhuria na wakenya zaidi ya elfu 10 katika wanja wa Wajir Stadium, rais William Ruto ambaye ni amri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi nchini, amesema atahakikisha sherehe za kitaifa zinafanyika katika kaunti mbalimbali nchini kinyume na ilivyokuwa miaka ya nyuma.
Katika hotuba yake kwenye sherehe hizo za Madaraka, Rais Ruto amesema tangu taifa la Kenya kupata uhuru eneo hilo lilitelekezwa katika masuala mbalimbali ikiwemo utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Rais William Ruto awaongoza wakenya kuadhimisha sherehe za Madaraka kaunti ya Wajir
Rais Ruto pia alisema eneo hilo lilitengwa kwa miaka mingi kwa madai ni eneo kame na hakuna usalama wa kutosha.
“Katika uongozi wangu, nitahakikisha wananchi wa maeneo haya wanapata maendeleo sawa na wengine nchini, na niko na uchunguzi sana kuona watu wa Wajir wametengwa kwa miaka mingi na suala hili halitashuhudiwa tena na usalama utaimarishwa kwa wananchi wote”, alisema Rais
Wakati huo huo, Rais Ruto alisema kila jamii ina haki ya kunufaika na maendeleo nchini bila kubaguliwa na kuomba msamaha wenyeji wa kaunti ya Wajir kwa kutelekezwa kwa miaka mingi.
